Monday, August 1, 2016

HOFU YA MUNGU YATANDA: SHUHUDIA PICHA ZA WATU WALIOKUWA VICHAA, NA WENYE MAGONJWA SUGU YALIYOSHINDIKANA KUPONYEKA WALIVYOPOKEA UPONYAJI WA PAPO KWA HAPO KWA MCH MZOLA WA NYAKASANGWE...!

0 comments
 Pichani Mchungaji wa Kanisa la Hossana Ngome ya Yesu lililopo Wazo Nyakasangwe akiwa picha ya pamoja na watu waliopokea uponyaji baada ya maombi yake huku watu hao wengine walikuwa vifaa kabisa lakini kwa sasa wamerejea kwenye hali yao ya kawaida.

Maelfu ya wananchi wenye uhitaji wameendelea kumiminika kwenye kanisa la Mchungaji Mzola kwa ajiri ya kumuona MUNGU wa kweli mbele za mtumishi huyu wa Mungu.
Mchungaji Mzola.
Na Mwandishi Wetu
Wakazti wa Jiji la Dar na vitongoji vyake wameendelea kukumbwa na mshangao kufuati miujiza ya Mungu inayoendelea kwenye kanisa la Mchungaji Mzola lililopo Wazo Nyakasangwe.
Mungu amekuwa akimtumia mchungaji huyu kufanya mambo ya kutisha kiasi cha kuwashangaza watu wengi ambapo hadi sasa watu wenye maradhi sugu kama ukimwi, kisukari, kansa na walio na ugumba, utasa, vifaa na wenye matatizo kwenye ndoa zao pamoja maofisini katika ajira zao wamefunguliwa na kupata ulinzi wa roho mtakatifu na sasa mambo yao yanakwenda vizuri.
Mtumishi huyo wa Mungu amekuwa na karama kubwa inayotokana na aliyemo ndani yake ambae ndiye anaeponya watu bali si yeye kwa maana Mungu yupo ndani ya kinywa cha mtumishi huyo hivyo kila atakalolitamka kwa jina la Yesu basi hata kama mtu alikuwa anasumbuliwa na aina yoyote ya tatizo basi anapokea uponyaji wa popo kwa hapo.
Mtumishi huyo ameendelea kuwasihi watanzania wasiache hadi mauti yawafike au jamaa zao wafe kwa ajiri ya maradhi hapana lipo tumaini pekee ambalo ni Yesu Kristo anaepatikana Kanisani kwake ambaye tiba na dozi yake ni ya uhakika mara moja tu basi mgonjwa anakuwa huru hivyo anayehitaji kuuona mkono wa Mungu utakaosambaratisha fitina kazini kwako, magonjwa yako na mikosi yako basi awasiliane na mtumishi huyo kwa simu namba +255 713 161 785 ni namba ya mtumishi huyo mwenye karama kubwa aliyopewa na MUNGU.

SOMA ZAIDI ...

Tuesday, July 26, 2016

KIMENUKA: UKAWA KWAWAKA MOTO, WAFUASI WA VYAMA HIVYO WAWASHUKIA MEYA WA JIJI/KINONDONI, HALIMA MDEE AHUSISHWA NA TATIZO HILO..!

0 comments



Mstahiki Meya wa manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob "UKAWA"
Mheshimiwa  Halima Mdee Mbunge wa Kawe- CHADEMA

Mkuu mpya wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi Salum

Isaya Mwita wa Chadema, Meya wa Jiji la Dar es Salaam "UKAWA" 
Na Mwandishi wa Maskanibongotz

Mashabiki na wafuasi wa vyama vilivyoungana UKAWA wamekuja juu na kuwataka viongozi wao wanashikiria nyazifa mbalimbali za kuwaongoza wananchi waachane na maneno badala yake wapige kazi ionekane ili wananchi waendeee kuwa na imani nao.
Wakiongea na mwandishi wetu juzi maeneo ya Kinondoni jirani na yalipo makao makuu ya Chadema walisema kuwa " Ndugu mwandishi sisi ni wafuasi wa Ukawa lakini kwa sasa tunachowataka viongozi wetu waingia mtaani kutatua matatizo ya wananchi na kero zao kwa vile wanamamlaka ya kufanya hivyo kutokana na nafasi walizonazo" Alisema 
Timoth Nyang'andu ambaye anatokea mkoani Singida.

Wafuasi hao waliongeza kusema kuwa kwa sasa viongozi hao waachane na habari za malumbano na Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa kupinga kauri anazozitoa kwa maana kufanya hivyo ni sawa kama wamekosa mawazo endelevu ya kuwasaidia wananchi.
Mashabiki hao wameomba Mwenyekiti wa Chama hicho Kitaifa Mheshimiwa  Freeman Mbowe atumie mamlaka aliyonayo kuwasihi viongozi waliopo chini yake nchi nzima kuachana na malumbano wapige kazi 2020 sio mbali kwani CCM wanajipanga kurudisha nafasi hizo hivyo njia watakazopitia CCM ni kuangalia mapungufu yaliyofanywa na Mamea hao nk.
Wakipiga mfano mgogoro wa Nyaksangwe kata ya wazo ambao kimsingi ni kama umemalizika kutokana na pande zote kati ya wenye mashamba na wakazi hao kukubaliana kumaliza hivyo ni nafasi pekee ya mamea  Isaya Mwita wa Chadema, Meya wa Jiji la Dar es Salaam "UKAWA"
Mstahiki Meya wa manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob "UKAWA" na Halima Mdee wanaweza kutumia nafasi hii vizri ya kushika nyazifa hizo kumaliza mgogoro huo uliouwa watu wengi sana miaka 7 iliyopita.
Halima Mdee Mbunge wa Kawe mgogoro huu unamuhusu sana kutokana na kuwa eneo lake na anaufahamu vizri mgogoro huu na anajuwa kabisa kama wapiga kura wake waliwahi kupoteza maisha wakigania haki yao hivyo ahusishwe  pamoja kumaliza tatizo hilo ambalo Mheshimiwa Makonda walishaweka njia nzuri ya kumaliza mgogoro huo.

Mstahiki Meya wa manispaa ya Kinondoni Boniface Jacoblicha ya hivi karibuni kufanya ziara ya kushtukiza kwenye eneo hilo lenye mgogoro na kupokelewa na maelfu ya watu na kujione auharibifu mkubwa uliofanywa na mafisadi ardhi hao waliotumia pesa zao kuwaangamiza wananchi hao kwa kutumia Jeshi la Polisi na mabaunsa na aliahidi kama miezi miwili isingepita ofisi yake ingeanza kugawa hatimiliki ya viwanja hivyo kwa kila mkazi mwenye eneo hilo ili watu wawe na uhakika na viwanja vyao lakini hadi leo kimya.
Source: Maskanibongotz
SOMA ZAIDI ...

Wednesday, July 20, 2016

KAZI YA KUPAMBANA NA MACHANGU/MASHOGA: RC MAKONDA APIGWA CHANGA LA MACHO, YANAYOFANYIKA KWENYE VITUO VYA MASSAGE DAR AIBU, MACHANGUDOA WAENDELEA KULA VICHWA KAMA KAWA...!

0 comments
Kufuatia kauri na msimamo wa mkuu wa Mkoa wa Dar Mheshimiwa Paul Makonda kutangaza kiama kwa machanguoa na mashoga, sasa wakina dada hao wamebuni nyingine ya kujiingiza kwenye vituo vya massage ambako huko wameendelea kula vichwa kama kawaida, Lakini uvaaji kama huu pichani umekuwa chanzo cha ngono kwa sababu huchochea hisia za kwa wanaume.
Unapoiingia sehemu ya Massage unakutana na wakina dada kibao unakaribishwa kuchagua mtu wa kukupa huduma.

Moja ya kituo cha Massage Jijini Dar
Na Mwandishi wa Maskanibongotz
Mkuu wetu wa mkoa anakazi ngumu na kubwa ya kutekeleza  agizo lake ambalo linapaswa kusimamia na Jeshi la Polisi kutokana na machangudoa hao kubuni mbinu mbadala ya kukwepa mkono wa dola.
Maskanibongotz umefanya uchunguzi na kubaini kuwa huko kwenye vituo vya massage baadhi vinafanya biashara ya ukahaba kabisa kwani kilichofanyika ni kusajir kazi ya massage lakini ndani yake hakufanyiki massage peke yake bali ni ufusika wa kufa mtu.
Vituo vingi vilivyopo hasa Kinondoni, Sinza, Mikocheni vimejaa balaa, Msasani, Kinondoni Hananasif ndani yake kuna wasichana warembo ambapo kila mteja akiingia hupewa nafasi ya kuchagua msichana anaempenda ili akamfanyie massage lakini na ngono pia.

Bei ya massage hizi za kawaida ni tsh 30,000/ na Ngono huwa ni makubaliano kutokana na aina ya ngono unayoiihitaji mteja na kuna aina nyingi ya ngono wanazozifanya wanawake hao, moja kuna kuna ngono ya mwanaume kuchezewa uume bila kufanya mapenzi hadi anamaliza haja yake, mbili mwanaume kunyonywa uume wake hadi anamaliza haja yake na mwisho kufanya mapenzi kabisa hizo aina zote zina bei tofauti.
Na wanaume wengi imegundulika hupenda kwenda huko kwa vile ni sehemu salama, wananchi wengi wamemuomba mkuu wa mkoa kuangalia upya uhalali wa kuwepo vituo hivyo kwa vile vingi vimekuwa madanguro ya kufa mtu.
Source: Maskanibongotz
SOMA ZAIDI ...

Monday, July 18, 2016

RC MAKONDA AFAFANUA ALICHOMANISHA KUHUSU MSAKO WA NYUMBA KWA NYUMBA KUIBAINI WAKAZI NA MAJUKUMU YAO, WANASIASA WANAOMPINGA WAWACHUKIZA WANANCHI..!

0 comments


Na Livingstone Mkoi
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda ametolewa ufafanuzi kuhusu upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya viongozi wa kisiasa dhiti ya maagizo mbalimbali anayokuwa anayatoa kwa ajiri ya kuijenga Dar Es Salaam mpya.
Akiongea na mtandao wa maskanibongotz Mheshimiwa Makonda alisema "Sikusema wasio na kazi wakamatwe. Utawapeleka wapi? Una gereza gani? Nilisema Wenyeviti wa mitaa wahakikishe wanawafahanu watu wao vizuri na shughuli wanazofanya. Wakitilia shaka nyumba fulani wachukue polisi kukagua na sio kukamata wasio na kazi kama inavyopotoshwa.." Alisema Makonda
Aidha Mkuu huyo wa mkoa aliongeza kusema kila agizo alilolitoa litakwenda kutekelezwa na  kuhusu na tayari vyombo vya usalama hasa Jeshi la Polisi limeanza kutekeleza agizo la Serikali.
Aidha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kinondoni Christopher Fuime aliueleza mtandao huu kuwa tayari wanashikiria vifaa vya shisha pale Oysterbay Polisi na msako mkali unaendelea kukamata machangudoa kwenye madanguro na wa barabarani ili kutimiza agizo la RC Makonda.
Hata hivyo wakazi wengi wa Jiji la Dar wamesikitishwa na kauri ya Meya wa Jiji la Dar aliyoitoa hivi karibuni ya kupinga agizo la Makonda ambalo kiukweli liko wazi na linaonekana kuwa na faida kwa jamii nzima ya Dar kwani mfano agizo la kuorozeshwa kwa wakazi wote kwenye nyumba wanazoishi na majukumu yao hali hiyo italeta faida kubwa kwani uharifu umekuwa mwingi kutokana na watu kuishi kiholela.
Wananchi hao wameomba wanasiasa kuacha kuacha kuingilia majukumu yenye faida kwa watu wengi kuliko wao
wanasiasa wachache.
Paul Makonda (RC Dar).!
SOMA ZAIDI ...

Tuesday, July 12, 2016

WAGONJWA WA UKIMWI, KANSA WAZIDI KUPOKEA UPONYAJI KANISANI KWA MCHUNGAJI MZOLA MWENYE NGUVU ZA AJABU ZA KIMUNGU, MAELFU YA WATU WAZIDI KUJISALIMISHA ILI KUJIOKOA NA KIFO, WATANZANIA WAONYWA KUHUSU KUBEZA WATUMISHI WA MUNGU..!

0 comments
 Mmoja wa wagonjwa wa Ukimwi aliyechelewa kuanza tiba akiwa ameathirika na vidonga kwenye kinywa chake, ambapo wagonjwa kama hawa wamekuwa wakipokea miujiza kwa mchungaji mzola wa Kanisa la Hosana Ngome ya Yesu Nyakasangwe kwa Mch Mzola.
  Bint wa shule mwenye maambukizi ya ukimwi.
   Mmoja wa wanandoa mwenye maambukizi ya ukimwi akipata ushauri wa Daktari kwenye moja ya Hospital za hapa nchini.
 Muuguzi akijua hali ya mgonjwa wake anayeugua ugonjwa hatari wa ukimwi. Ambapo wagonjwa wengi kwa sasa wameacha vitanda mahospitalin na kukimbilia kwa Mch Mzola wa Kanisa la Hosana Ngome ya Yesu Nyakasangwe Wazo Jijini Dar Es Salaam.
Hiki ndiyo kirusi cha ukimwi kama kinavyoonekana.

Mgonjwa ukimwi ambaye ni msanii aliyewahi kuwa na jina kubwa kiasi akiteseka na maradhi haya nyumbani kwao Arusha.


Na Mwandishi wa Maskanibongotz
Maajabu makubwa yameendelea kutendeka kwa Mch Mzola wa Kanisa la Ngome ya Yesu kwa watu wenye magonjwa mbalimbali waaminio   kwa kupokea uponyaji wa haraka kiasi cha kushangaza wengi.
Mungu amekuwa akimtumia mtumishi huyo kutenda miujiza ambapo hadi sasa maelfu ya watu wameendelea kumiminika Kanisani kwa mchungaji huyo huku wasiokuwa na uwezo wa kufika Kanisani kwake wakipokea uponyaji kupitia simu zao huko wlaiko.
Mchungaji Mzola toka igundulike nguvu ya aina yake aliyokuwa ya kiroho ya kuwaombea watu na wakapokenya uponyaji basi hali imekuwa tete Kanisani kwake ambapo kila siku za Mungu maelfu ya watu humiminika na kupokea uponyaji wa kweli.
Akiongea kwa simu namba 0713-161785 Mch Mzola alisema " Ndugu waandishi Mungu aliyepo mahara hapa si wa mzaha anatenda kazi zake kwa uadilifu mimi siponyi watu anayeponya ni Mungu hivyo ukifika hapa sisi tunachokifanya ni kukupa dozi mara moja na Mungu hushusha maajabu yake na unapona kamwe huwezi kuja hapa mgonjwa ukaondoka mgonjwa hapa Dakatari aliyepo hapa ni kiboko ya madaktari" Alisema Mch Mzola.
Hata hivyo mchungaji huyo anasema amekuwa akipokea wagonjwa wengi sana wenye magonjwa sugu kama Ukimwi, Kansa, Kisukari, na wenye matatizo kama ganzi, kupooza, umasikini, kushindwa kuolewa/kuona/ kufanikisha ndoto zako, wanafunzi kufanya vizuri darasani, wanaotafuta kazi bila mafanikio hao wanapata dozi maalum ndani ya wiki moja majibu wanayapata. na mengineo mengi.
Mchungaji huyo anasema ndugu na jamaa wenye ndugu zao ambao wako hali mbaya hawajiwezi wawabebe hata kwenye machela na kuwafikisha Kanisani kwake ila kwa wasioweza kufika kabisa Kanisani kwake basi wapige simu yake hii 0713-161785
 ambayo inapatikana masaa 24.


Hata hivyo mkazi wa Jijini Dar Thomas Jonson 45 ametoa angalizo kwa binadamu wote kuacha tabia za kubeza watumishi wa Mungu ambao uwepo wao duniani wanamuwakilisha Mungu hivyo si vyema sana kuwabeza, iwe mashekh sharif, Mashekh na wachugaji inapotokea wakawa wanafanya mambo ya uponyaji kama huu anaoufanya Mch Mzola kama hawataki kuamini ni heri kukaa kimya kuliko kuwasema vibaya watumishi hao wanaweza kujikuta kwenye laana nzito.

MUNGU hashindwi Jambo na lisilowezekana kwa wanadamu litawezekana kwke. Uponyaji wa kweli unatoka kwa Mungu. Karibuni sana kuja kupokea uponyaji wa kweli.
 Mch Mzola akiwa Kanisani kwake Nyakasangwe kata ya Wazo
SOMA ZAIDI ...

Wednesday, July 6, 2016

BAADA YA KUAPISHWA JANA: MKUU WA WILAYA KINONDONI AAPA JAMBO ZITO , AANDALIWA MAPOKEZI YA KUFA MTU MITAA YOTE KUSIMAMA KWA MUDA...!

0 comments
 Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Salum Hapi Ali ameapa kufuata nyayo za Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kwenye kutatua tatizo la migogoro ya ardhi na tayari ana kamati maalum inayojumuisha watu wa mipango miji,maafisa ardhi hivyo kazi hiyo itaanza mara moja, DC huyo aliongea hayo juzi wakati akiapishwa tayari kuanza majukumu yake kwenye Wilaya hiyo yenye wajanja wajanja wengi hasa wenye fedha ambao wamekuwa wakiwaonea watu wanyonge. Lakini hata hivyo kwa sasa Jiji zima la Dar kwa  macho yote wameyaelekeza Kata ya Wazo kwenye mitaa ya Nyakasangwe na Kaza Roho ambako RC Makonda tayari alikuwa amefikia mahara pazuri za kumaliza mgogoro huo uligharimu maisha ya watu zaidi ya 13 huku wakina mama wakijifungua kabla ya siku zao na watoto zaidi ya 250 kupoteza masomo yao kutokana na watu wanaojiita wenye mashamba kutumia pesa zao kuwashika viongozi wa Polisi na wilaya kisha kujichukulia sheria mikononi bila kibali cha mahakama na waliweza kwenda kuvunja tu nyumba za watu na kuwatia umasikini mkubwa.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyakasangwe na Kazaroho Mch Peter Bilebela akiongea na maelfu ya wananchi wa mtaa wake waliokuwa wanamsubiri Makonda kwenye moja ya mikutano yake ya kuwatete wananchi wanyonge.
Rais Dk John Pombe Magufuli ameombwa pia kuangalia kwa jicho la tatu mgogoro wa Nyakasangwe na kuwaongezea meno RC Makonda, RC Kinondoni, kwani ndani yake kuna baadhi ya watumishi wa Serikali walihusika kuwaonea wapiga kura wake hali iliyopelekea wakazi hao zaidi ya 5000 kukosa imani na Serikali yao hadi hivi karibuni alipokuja Makonda kurudisha imani kwa wakazi hao na kubaini kama wapo baadhi ya watendaji toka Mipango Miji Manispaa ya Kinondoni walihusika kwa kiasi kikubwa kuwaonea wananachi hao wanyonge kiasi cha kuwaita wakimbizi ili waondolewe maeneo hayo waliyopewa na Mkuu wa Mkoa Miaka mingi iliyopita baada ya msitu huo kuwa tishio kwa usalama wa wananchi.

 Marehemu Chura ambaye alikuwa kiongozi wa mabaunsa aliyekuwa upande wa wenye mashamba kwenye harakati za kuwaondoa wananchi hao wa Nyakasangwe  kinguvu, hali iliyopelekea vita kubwa kuibuka huku baunsa zaidi ya watatu kufariki kwenye mapambano hayo licha ya kwamba walijitahidi kwa kukimbia lakini mwisho wa siku waliishiwa pumnzi kisha wakakamatwa na kuanza kukatwa katwa mapanga
RC Makonda alivyopokelwa na Mabango yakimtaka kuondoa mtandao wa ufisadi kwenye kitengo cha Ardh Kinondoni ambao wanadaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo kwa kuhodhiwa na wenye mashamba wenye pesa chafu.
Na Sakina Sahaban
Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Salum Hapi Ali ameapishwa juzi tayari kuanza kuitumia wilaya ya Kinondoni huku macho, masikio ya wakazi wa Jiji yakielekezwa Kata ya Wazo mitaa ya Nyakasangwe na Nyakalekwa ambako kuna shida sana huku rekodi zikionesha ndiko kulikopoteza maisha ya watu wengi kwenye mgogoro wa ardhi.
Watu wanaodaiwa kuwa wenye mashamba wamekuwa na nguvu kubwa ya kifedha na wameshika idara zote kabla ya Makonda hajawa DC Kinondoni na alipokuja kidogo nguvu hiyo ya uonevu wa wazi ilianza kufifia kutokana na msimamo mkali wa Makonda wa kutetea wanyonge.
Hata hivyo watanzania wengi wanaimani na Mheshimiwa Ali Salum Hapi Ali na wanaamini kuwa atawasaidia wakazi hao wa Nyakasangwe na Manispaa ya Kinondoni kushirikiana na Meya wake watawapatia wakazi hao hati halali za viwanja hivyo walivyopewa kihalali na Serikali ya Mkoa chini ya Makamba.
Pia kauri hiyo ya Mkuu wa Wilaya aliyoitoa imewapa matumaini wakazi wa Nyakasangwe huku wakiahidi kumuandalia mapokezi makubwa siku ya kwanza kufanya ziara ya kikazi kwenye mitaa yao huku wakiwa na matumaini makubwa na kiongozi huyo kijana.
Source; Maskanibongotz 

SOMA ZAIDI ...

Monday, July 4, 2016

KASI YA MAKONDA KIBOKO, CHADEMA WAUNGA MKONO MITAA KUPEWA JINA LA MAKONDA KWA HESHIMA NA KAZI NZURI ALIYOIFANYA, UKAWA WAMSHAURI HAYA MEYA KINONDONI...!

0 comments
 Pichani Mkuu wa Mkoa Dar kipindi akiwa DC Kinondoni akiongea na wananchi wa Nyakasangwe na kuwatia kuhusu Mgogoro huo wa Ardhi na kuahidi kutatua haraka tatizo hilo ili wananchi waishi kwa amani kama wakina ndani ya nchi yao.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob ambaye ameshauriwa na watanzania wengi hasa wakazi wa Jiji la Dar kushirikiana na mheshimiwa Makonda kumaliza tatizo la mgogoro wa Nyakasangwe ambao unaonekana unanuka rushwa zilizowahusishwa baadhi ya  watendaji wa mipango miji Kinondoni lakini pia hata ofisi ya Mkuu wa Mkoa kabla ya Makonda nao wamehusishwa na mgogoro huo kwa kushindwa kusimamia na kumaliza tatizo hilo.
Na Mwandishi Wetu. Wazo
Wanachama wa Chema Wilaya na Kinondoni wameunga mkono maombi ya wananchi wa mtaa wa Nyakasangwe na Nyakalekwa kutaka mitaa hiyo kuitwa jina la mheshimiwa Makonda na kusema anastahir kwa kazi aliyoifanya.
Wakiongea na maskanibongotz wananchama hao pia wanaunda Ukawa walisema" Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpenzi Makonda anastahiri heshima kwa kazi nzuri aliyoifanya kwenye mgogoro huu wa ardhi" Alisema kijana mmoja ambaye ni kata wa kutupwa wa Chadema
Aidha wananchama hao waliendelea kusema kuwa amani inayooneana sasa Nyakasangwe yenye wakazi zaidi ya elfu tano ni kazi ya Makonda ambaye amefanikiwa kufanya kitu kilichowashinda viongozi kiba " Jamani ili kwa hili hakiaka sisi kama wapinzani tunaunga mkono maombi haya ya mitaa hii kupewa jina la Makonda kwa vile anastahiri hivyo na ili hata vizazi vijavyo vije kutambua mchango  mkubwa uliofanya na kiongozi huyo mpenda haki na mtetezi wa wanyonge" Alisema Mama zainabu
Mheshimiwa Makonda ambaye mara kadhaa katika mikutano yake Nyakasangwe amekuwa akiwatia moyo sana wananchi hasa wakina mama hao na kuwafananisha na Mama yake mzazi lakini pia na maisha aliyokulia mheshimiwa huyo ni hali ya chini hivyo amekuwa akiwambia wakazi hao wasiwe na shaka iko siku maandiko yatatimia na wataishi kwa matumaini huku wakiwa na hati zao.
Wadau mbali mbali wamemshauri Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob kuwa makini na ataarifa anazozipokea toka kwa watendaji wake hasa wa Wazo ambao wamekuwa wakimpa taarifa tofauti juu ya mgogoro huo ambao kimsingi ni kama umeisha, huku kukiwa na taarifa kama viongozi hao wana bifu za kisiasa na mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyakasangwe Mtumishi wa Mungu Pete Bilebela wa CCM.
Sourc: Maskanibongotz
SOMA ZAIDI ...

Saturday, July 2, 2016

MUNGU WA KWELI AJIDHIHIRISHA KWA MCHUNGAJI HUYU, MCHUNGAJ MZOLA ATAKA KULETEWA VICHAA, MATASA, WENYE UKIMWI, KISUKARI, NGUVU ZA GIZA, MAELFU WAZIDI KUMIMINIKA KANISANI KWAKE...!

0 comments

 Hii ndiyo taswira ya waumini wanaendelea kupokea uponyaji wa kweli toka kwa mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Ngome ya Yesu lililopo Nyakasangwe Wazo.

 Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Ngome ya Yesu akiendesha ibada kwenye Kanisa lake


Na Amina Saidi- Maskanibongotz
Yule mchungaji kiboko ya wachawi nchini Tanzania Mch Mzola wa Kanisa la Hosana Ngome ya Yesu ameendelea kuwaasa wakazi wa Jiji la Dar na hata mikoani kuendelea kumpelekea watu wenye matatizo sugu yaliyoshindikana huko kote hata kwa wachungaji wengine.
Akionge jana kwenye ibada ya maalum ya kumuombea Rais Magufuli,Paul Makonda na Waziri Lukuvi ili kuendelea kuguswa na mgogoro wa ardhi ulioua watu zaidi ya 23 hadi sasa.
Mchugaji Mzola amesema anashukuru kumekuwa na muitikio mkubwa toka kwa wakazi wa Jiji la Dar ambayo wengi wamepokea uponyaji wa kweli na sasa mambo yao yamekaa vyema na Mungu amewabariki.
Mcungaji huyo amesema watu waendelee kuwaleta jamaa zao wenye magonjwa sugu na watapokea uponyaji wasioutegemea kwa maana Mungu wake yeye ni mungu wa kweli na uzima na ni MUNGU asiye babaisha hivyo wote wanahitaji tiba hiyo toka kwake  wafike kanisani kwake matibabu na dozi zake ni bure tu kumpa mungu utukufu tu ndiyo malipo yake .
Mchungaji huyo aliongeza kusema kuwa anaendelea kutoa uwito kwa watanzania wote kuendelea kufika Kanisani kwake ili wapate uponyaji, kwani Kwa Mungu hakuna lisilowezekana, kila magonjwa yote sugu, ugumba, utasa, mikosi ya kushindwa kuolewa/kuona, kuwa na mashaka, hofu ya kifo nk.
Na amesema watkaoshindwa kufika kanisani kwake Kata ya Wazo mtaa  Nyakasangwe wanaweza kumpigia simu kupitia namba hizi 0763-161785/ 0713-161785 na wao watapokea uponyaji huko walipo.  
SOMA ZAIDI ...

Tuesday, June 28, 2016

KIMENUKA: RAIS MAGUFULI, PAUL MAKONDA NA LUKUVI WAZUSHA HOFU, MAJINA YA MAFISADI ARDHI KATA YA WAZO WANAODAIWA KUUWA WANANCHI WASIOKUWA NA HATIA KUTUA MEZANI KWA MH RAIS. VIONGOZI WA DINI WAWAOMBEA MSAMAHA WENYE MASHAMBA WALIAMUA KUWAACHIA WANANCHI...!

0 comments
 Mkuu wa Mkoa wa Dar Mheshimiwa Paul Makonda ambaye inadaiwa anataarifa kamili kuhusu mgogoro huo kutokana na mafanikio makubwa aliyofikia ya kuleta amani na mshikamano kwa pande hizo mbili watu wenye mashamba na wananchi wakazi wa maeneo hayo.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akikagua utendaji wa watumishi wa Mipango Miji na Ardhi Wilayani Ilemela., ambapo wakazi wa Nyakasangwe nao wanaimani na Mheshiwa Lukuvi iko siku moja atakuja kufanya maamuzi magumu.
Aliyekuwa kiongozi wa mabaunsa ambaye kwa sasa ni marehemu aliyefahamika kwa jina moja la Chura, picha ikionesha jinsi alivyokatwa mapanga kwenye mgogoro huo wa ardhi uliotokana na mafisadi kutumia mabaunsa hao kuvunja nyumba na wananchi bila kibali halali mcha mahakama na kusababisha vita kubwa na kupelekea vifo vya mabaunsa hao na wananchi.

Dokta John Pombe Magufuli Rais wa Tanzania ambapo Serikali yake kwa sasa imerusha matumaini mapya kwa wananchi kutokana na utendaji wake kazi wa haki na kuwatetea wapiga kura wake, hali hiyo ikizusha hofu kwa watu wenye fedha waliozoea kuwaone wananchi kwa fedha zao, ambapo jambo hilo kwenye Serikali hii limekuwa gumu huku Rais akiwa mstari wa mbele kupambana na ufisadi wa kila aina, Hali hiyo imeendelea kuwapa matumaini wakazi Wazo mitaa ya Nyakasangwe na kuamini iko siku maandiko yatatimia kwa Serikali kufanya maamuzi magumu ya kuwakamata mafisadi ardhi wote waliofanya uharibifu na kuua wananchi.
 Na Livingstone Mkoi

Utendaji kazi wa haki na uwazi unaofanywa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais  Dk John Pombe Magufuli umeleta matumaini mapya kwa wakazi wa kata ya Wazo kwenye mitaa ya Nyakasangwe na Nyakalekwa wanaoongozwa na Mwenyekiti wao Mch Peter Bilebela ambao kwa muda mrefu  wamekuwa wakipata shida na kujiona kama vile si Watanzania kutokana nak kile kinachodaiwa kukosekana kwa uaminifu kwa baadhi ya watumishi wa Serikali ambao walikuwa wanatumiwa na baadhi ya watu wenye fedha nyingi au maarufu kwa majina ya mafisadi ili kuwaonea wananchi hao huku wakiitwa wavamizi na wakimbizi.

Wananchi hao walikosa imani na baadhi ya viongozi wa Serikali ya awamu ya nne ambao wanadai ni kama walifanikiwa kuhodhiwa na matajiri hao hivyo ofisi ya Mkuu wa Mkoa iliyokuwa inaongozwa na Bw. Saidi Meck Sadiki, ofisi ya Mkuu wa Wilaya iliyokuwa inaongozwa na Mheshimiwa Jordan Lugimbana , Meya wa Kinondoni, Yusuf Mwenda na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Mussa Natty, Jeshi la Polisi Kanda Maalum hivyo kushindwa kumaliza tatizo lao la mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wakazi wa mitaa hiyo na watu wanaojiita wenye mashamba hali iliyopelekea badala yake utatuzi kuelemea upande mmoja na ilitumika nguvu kubwa toka Jeshi la Polisi Kanda Maalum lililokuwa likiongozwa na Suleiman Kova  kuwahamisha wakazi hao mara moja kwa amri toka ofisi ya mkuu wa Mkoa kwa madai kuwa watu hao ni wavamizi.


 Zoezi hilo ambalo lilihusisha silaha za moto huku matajiri hao wakihusishwa kugharamia mafuta na posho za zilizonona kwa walioendesha zoezi hilo,kitu ambacho kilipelekea vita kubwa kuibuka na wananchi walichezea kichapo cha mbwa mwizi, huku mali zao zenye thamani ya mabilioni ziliharibiwa vibaya, watoto wakikosa pa kujificha huku watu zaidi ya kumi na tatu wakipoteza maisha kwenye mapambano hayo ya ugomvi wa ardhi hivyo kupelekea kuibukakwa uhasama  kati ya raia na Polisi, watu wa manispaa kiasi cha kufanya eneo hilo lile gumu kuingilika na jeshi la Polisi bila kuwa na silaha za moto kwani Wananchi hao walikuwa wanatamani kuwadhuru.

Maskani linatambua kuwa mtu aliyemaliza mgogogro huo ni Mheshimiwa Paul Makonda kipindi hicho akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambapo alifanikiwa kurudisha hali ya amani kiasi cha kuwashangaza hata viongozi wengine waliokuwa wameshindwa kufanya hivyo ambapo hadi sasa wakazi hao wameendelea na shughuri zao za ujenzi wa taifa licha ya kwamba bado wakazi wengi hawajapatia hati miliki za viwanja wanavyoishi kutokana na baadhi ya watu wanaojiita wamiliki  kuendelea kung'ang'ania kama wana haki na maeneo hayo ambayo sio mashamba tena kama wanavyodai bali yameshakuwa makazi ya watu. 


Hata hivyo zoezi la mwisho kwenye mgogoro huo ilikuwa kwa wakazi hao kuhakikiwa majina na viwanja wanavyooishi, lakini kuna baadhi ya watu waliokuwa kwenye idadi ya watu wanaosema makazi hayo yalikuwa mashamba yao ambao ni Rajabu House na Bwana Pius wao kwa moyo mkunjufu walitangaza kuachana na mgogoro huo hivyo maeneo yao ambayo yalikuwa msitu mkubwa kabla ya wananchi kupewa na Mkuu wa Mkoa mstaafu Mheshimwa Yusuph Makamba wayaendeleze baada ya kuwa maficho ya wezi, hatua ambayo imepongezwa na watu wengi wakiwemo viongozi wa dini na vyama vya Siasa kwa vile taarifa za ndani kabisa zinadai vyombo vinavyohusika na mambo ya usalama kwa sasa vinaendelea na uchunguzi juu ya jambo hilo na kubaini watu hao wenye mashamba walipata wapi mamlaka ya kumiliki na hata kusababisha vifo vya watu na kuharibu mali zao.

Wakiongea na maskanibongotz viongozi hao wa dini waishio eneo hilo ambao na pia ni wahanga wa kuvunjiwa, Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Lililopo Nyakasangwa alisema " Uonevu uliofanyika kwa wakazi hawa wa Nyakasangwe pamoja na damu zao kumwagika sisi kama watumishi wa MUNGU tulisha mwomba yeye atoe hukumu kwa wote waliohusika na hili jambo, lakini tunamuomba Rais wetu mtukufu Mheshimiwa John Pombe Magufuli kuwasamehe hawa watu wenye mashamba waliosamehe vita hii ya mgogoro wa ardhi kwa vile tayari wametubu madhambi yao" Alisema Mchungaji Mzola.

Aidha  Shekh Saharif Khamis ambaye tangu mgogoro huo uanze amekuwa akiombea dua amani ili watu wasimwage damu, amefurahishwa na watu wenye mashamba waliosamehe maeneo hayo,  ‘Utendaji kazi wa haki unafanywa na Rais John Pombe Magufuli, Mheshimiwa Paul Makonda na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi huenda ndiyo uliopelekea baadhi ya watu hao wanajiita wenye mashamba kuamua kuachana na mgogoro huo kutokana na misimamo mikali ya viongozi hawa wapenda haki, ambapo hadi sasa kimya chao kuhusu sakata hili la ardhi ambapo Mheshimiwa Makonda ana picha nzima ya mgogoro huo kutokana na kamati yake aliyoiunda wakati akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni huenda kikawa na mshindo mkubwa siku yeyote maamuzi magumu yanaweza kufanyika kumaliza mgogoro huo wa ardhi ili wananchi waendelee kurudisha imani kwa Serikali yao. 

Source: Maskanibongotz.



SOMA ZAIDI ...

Thursday, June 23, 2016

KASHFA NZITO!!!, BONDIA MAARUFU TZ MBARONI KWA KUKUTWA NA KETE 300 ZA BANGI NA MIRUNGI, ATUMIA VIBAYA JINA LA MH MAKONDA ILI POLISI WAMUACHIE, POLISI WAMKAMATA KIMAFIA, AFANDE MAKOMEO APONGEZWA NA WANANCHI..!

0 comments
  Hapa Bondia Dulla Mbabe akimuomba D/c1090 Thausen Mwamba maarufu Makomeo amuachie huru kwani kama taarifa hizo zitawafikia viongozi wa chama cha ngumi kinachomuongoza atafungiwa hali inayoweza kumuua njaa.

  Bondia Dulla Mbabe kushoto akiwa na Mada Maugo siku walipopima uzito kwa ajiri ya pambano lake.
Mheshimwa Makonda ambaye jina lake limetumiwa vibaya na Bondia huyo ili Askari  D/c1090 Thausen Mwamba maarufu Makomeo  amuachie huru kwa kosa hilo



  Kote za bangi na mirungi anazodaiwa kukutwa Bondia Dulla Mbabe.
  D/c1090 Thausen Mwamba maarufu Makomeo akimbana kwa maswali Dulla Mbabe ambae amevishwa pingu kituoni hapo.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar, Simon Sirro
 Rais wa chama cha ngumi za kulipwa Tanzania TPBC (Tanzania Professional Boxing Commission) Chaurembe
 Rais wa Chama cha Ngumi za KUlipwa TPBO Yasin Abdalah
Rais Wa PST Emanuel Mlundwa


Na Zainabu Khatibu-Maskanibongotz

Katika hali ya kushtua Bondia maarufu wa uzito wa juu Tanzania anayefahamika kwa jina la Dulla Mbabe anashikiriwa na Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni kwa tuhuma za kukutwa na Mirungi na kete zaidi ya 30 za bangi.

Tukio hilo la aina yake lililotokea maeneo ya uwanja wa mpira uliopo Mwanyamala Jijini Dar saa 2:30 za usiku wakati polisi hao wakiwa kwenye msako mkali wa kupambana na uharifu ndipo na Dula alipokutwa eneo hilo. 
Mmoja wa askari aliyeshiriki kumkamata Dulla alisema siku hiyo wakiwa kwenye patro ili hali wakijua uwanjani hapo wahuni wengi hupenda kukaa mara baada ya mazoezi ya mpira ndipo mkuu wa oparasheni kata ya  Makumbusho Kopro Makomeo toka kituo cha Polisi Mwananyamala  alipopanga vijana wake kuzunguka uwanja huo kabla ya kuvamia.
Mashuhuda wa tukio hilo wameieleza Maskanibongotz kwamba baada ya Mkuu huyo wa Oparesheni  huyo kuweka sawa vijana wake ambao wengi ni Polisi jamii wenye mazoezi makali ya michezo yote walipoanza kuvamia eneo hilo, baadhi ya wahuni walifanikiwa kuwatoka Polisi hao kumuacha Dulla, ambaye pamoj na kujaribu kukimbia alinasa katika mikono ya D/c1090 Thuasen Mwamba maarufu kama Makomeo mbaye yupo fiti kila idara alifanikiwa kumpiga mtama uliompaisha kimo cha Ng'ombe na kudondokea kiuno.
Pamoja na mtama huo, lakini Dulla alifanikiwa kunyanyuka na kukimbia hadi nje ya uwanja na kutupa mirungi lakini baada ya muda kutaka kujifanya amewazoea Polisi akarudi na kuanza kuwahoji Polisi nani aliyempiga Mtama, kitu ambacho kiliwafanya Polisi hao kumuuliza kwa nini alikimbia kama si Mharifu, lakini kama alihisi amewaweza Mapolisi, Dulla alizidi kuwajia juu Polisi na kuwatishia kuwapiga up cut za chembe, huku wahuni wengine nao wakipata nguvu ya kurudi uwanjani hapo na kuwazunguka Polisi.

Lakini ili kuweza kuweka hali sawa askari mmoja alitoa bastola ambayo  ilisaidia kuwasambaratisha Wahuni wote ambao walirudi kuhakikisha wanakabiliana na Polisi hao huku nguvu wakizipata kutoka kwa Dulla ambaye baada ya tukio hilo alibaki tena peke yake na kutiwa Mbaroni pamoja na kujifanya kutishia kwamba yeye na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni marafiki kitu ambacho kilizidi kupandisha hasira  D/c1090 Thausen Mwamba maarufu Makomeo  ambaye kwa kushirikiana na vijana wake walifanikiwa kumvisha pingu Bondia huyo huku  anawatishia askari hao kama kuna kazi anataka kufanya na Mheshimiwa Makonda hivi karibuni ya kuchangia madawati kwa kucheza pambano lake na mmarekani. 
Tukio hilo liliendelea kuwa na sekeseke kwani baada ya kufunguliwa Pingu walipofika kituo cha Polisi Mwinyijuma, Dulla alifanikiwa kuwatoka Polisi hao lakini walifanikiwa kumkamatia eneo ya Kapakabana na kumpeleka moja kwa moja kituo cha Polisi cha Oysterbay na kumfungulia OB/RB/11362/16, kwa kosa la kupatikana na kosa la Bhangi na Mirungi.
Gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza na Bondia huyo wakati akiwa kituo cha Polisi CCM Mwinyijuma, ambapo bondia huyo alikana kukutwa na bangi hizo,pia gazeti hili lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda ya Kinondoni ili aweze kuzungumzia tukio hilo lakini  Kamanda huyo alikuwa kwenye kikao na kuomba atafutwe baadaye hadi tunakuletea taarifa hizi bado tulikuwa hatufanikiwa kumpata Kamanda huyo.

Aidha Wananchi mbalimbali wamezungumzia tukio hilo na kulaani vikali kwa bondia huyo kukutwa na madwa hayo, ila la pili kilichowasikitisha ni kutumia vibaya jina la Mheshimiwa Makonda na kuamini kama akisikia taarifa hizi na yeye atachukua hatua kali za kinidhamu kwani kujuana na Mheshimiwa isiwe chanzo cha kuvunja sheria za nchi na wanaamini pia chama cha ngumi kinachomuongoza bondia huyo pia nao watachukua hatua kali za kisheria dhidi ya bondia huyo itakapobainika kama kweli ametenda kosa hilo.

Wananchi walioshuhudia tukio hilo wakimuomba Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Paul Makonda kumtizama kwa jicho la tatu kwa kumpongeza Afande mwenye namba D/c1090 Thausen Mwamba maarufu Makomeo kwa ujasiri wa kumkamata Bondia huyo licha ya kumtishia kama yeye na Makonda ni  ndugu ili wasimkamate, lakini afande huyo alimkazia hadi kumfikisha kituoni na kumfungulia mashtaka.

 Source: Maskanibongotz.

 
SOMA ZAIDI ...

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king