Friday, June 17, 2016

BALAA KUBWA!!! MKUTANO WA MEYA KINONDONI CHUPUCHUPU, WANANCHI WAANGUA VILIO WAKIMLILIA RC MAKONDA, WAMTAKA WAZIRI LUKUVI KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU...!

0 comments
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi ameombwa kuingilia kati suala hilo kwa vile wanahisi kama ofisi ya Meya Kinondoni hili jambo la mgogoro wao wa ardhi wameuingaza kwenye siasa.
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Boniface Jacob ambae leo hii amezusha balaa kubwa Kata ya wazo kufutia wananchi kushindwa kumuelewa katika hotuba yake.
Mheshimiwa Paul Makonda akiwa amekaa chini pamoja na wakina mama wa Nyakasangwe na Kazaloho siku ya kwanza alipowatembelea kwa ajiri ya kutatua mgogoro huo wa ardhi uliopelekea mauji ya wananchi wasiokuwa na hatia huku wakina mama kadhaa wakijifungua kabla ya siku zao kwa mabomu ya polisi waliokuwa wanatumiwa na watu wenye mashamba kuonea raia.

Na Livingstone Mkoi
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mkutano wa kwanza wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Boniface Jacob katika Kata ya Wazo kwenye mitaa ya Kazaroho na Nyakalekwa nusra usimalizike baada ya wananchi hao kucharuka vibaya.
Mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwa mmoja wa watu waliohudhuria mkutano huo alishuhudia tifutifu hilo lililosababishwa na uchelewaji wa kiongozi huyo mkubwa katika Manispaa ya Kinondoni.
Mkutano huo ulianza saa nane mchana wakati wananchi wakifika eneo hilo toka saa moja asubuhi wakiwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Peter Bilebela.
Mkutano huo wa kwanza kwa Meya huyo Mheshimiwa Boniface Jacob ulikuwa na ajenda ya kiongozi huyo kuzungumza na wakazi hao kuhusu mgogoro wa ardhi ambao umesababisha vifo vya watu zaidi ya kumi miaka minne iliyopita ulitokana na watu wanaodai kuwa na mashamba kutumia polisi, na mabaunsa kuharibu mali na kuwapiga wananchi.
Hata hivyo mara baada  ya Mheshimiwa Boniface Jacob kuwasili eneo la uwanja wa Nyakalekwa CCM akiwa ameambatana na maafisa wa ardhi, akiwemo Diwani wa kata ya Hananasif, Mheshimiwa Kimbita, Diwani wa Kata ya Wazo na wengine moja kwa moja alilakiwa na umati mkubwa wa akina mama waliokuwa na matumaini tele ya kumuona kiongozi huyo kwa mara ya kwanza toka achaguliwe kuwa Meya.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyakasangwe, Peter Bilebela alifuata itifaki zote zinazostahili kwa kumkaribisha Diwani wa Kata ya Wazo ili amkaribishe mgeni rasmi na mara baada ya kumkaribisha Meya, akiwa ameshika kipaza sauti, alianza kuwasalimia wakazi hao na baadae kuwainua Maafisa Ardhi waanze kusema kwa nini zoezi hilo limechukua muda toka uhakiki umalizike.
Hata hivyo, katika hali ya kushtua, mmoja wa Maafisa Ardhi hao ambaye alitakiwa kuzungumzia suala hilo alianza kuongea kwa kubabaika hali iliyowafanya wananchi hao kuanza kunong'ona chini kwa chini na baadae kwa sauti ya juu hadi afisa huyo alipoamua kumpatia kipaza sauti Afisa mwingine wa Ardhi aliyeambatana Mheshimiwa Meya.
Ufafanuzi wa Maafisa Ardhi huo ulionekana kupingwa na wananchi kiasi cha kuchafua hali ya hewa, hali iliyomlazimu Peter Bilebela Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo kufanya kazi ya ziada ya kuwatuliza wananchi wake.
Meya alianza kuzungumzia kuhusu mgogoro huo akisema awali palitokea makosa kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya (DC Makonda) ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutowashirikisha viongozi wenzake kwenye suala la uhakiki aliofanyika, kauli hiyo pia ilitaarifiwa kama imeingizwa kwenye siasa.
Kwa sababu kipindi Makonda anafanya maamuzi ya kutatua mgogoro huo hakuwa amemshirikisha Mbunge ambaye ni Halima Mdee na viongozi wengine wa Chadema hivyo moja kwa moja wenye uelewa wa mambo walikuwa wameshamuelewa Mheshimiwa Meya huyo alichomaanisha.
Hata hivyo, Meya huyo alizidi kuzungumza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuwasihi watu wasiuze tena mashamba wala kuvamia maeneo mengine kwani kufanya hivyo ni kuendeleza migogoro, lakini, Meya huyo alienda mbali zaidi na kusema kuwa wananchi hao wasijione kama wao wana haki ya kumiliki ardhi hiyo kwa vile wenzao upande wa pili wenye mashamba wengine wana hati tayari za mashamba hayo.
Kiongozi huyo wa Kinondoni aliendelea kusema mengi huku mengine yakionekana dhahiri kuwa vijembe kwa Mwenyeketi Peter Bilebela, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, lakini, jambo lililozusha mtafuruku kiasi cha kuwafanya wananchi kushindwa kumvumilia na kuanza kumjibu katikati ya maongezi yake ni pale alipotoa kauli kwamba hadi sasa watu waliofika kwenye ofisi za ardhi wakitaka nao waorodheshwe kwenye majina ya uhakiki imefikia elfu moja.
Kauli hiyo ilionekana kupingwa vikali na wananchi hao pamoja na Mwenyekiti Peter Bilebela na kusababisha Meya huyo kuwa mpole mbele ya umati huo na kuwaeleza watu kama wanauza viwanja zaidi ya mara mbili basi waache kwa vile ana nia njema na wao na anataka hadi mwezi wa Desemba anahitaji wawe wamepata hati zao.
Baada ya hotuba hiyo ya Mheshimiwa Meya, kipaza sauti kilirudi kwa Peter Bilebela Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo na kumsihi Meya pamoja na Maafisa Ardhi kuwa ni lazima wafuate itifaki (protocal) kwani haiwezekani kwa yeye kama Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ambaye ni kama rais wa mitaa hiyo, kujua idadi ya wakazi wake wote na kuwa na orodha ya watu  wenye viwanja, hivyo, anashangazwa na hao watu elfu moja walioongezeka toka kwenye ile idadi ya wakazi wake elfu nne anaowatambua.
Hivyo, Peter Bilebela aliwasihi maafisa hao pindi wanapoona watu  wanaotaka kuvuruga amani ya mtaa wake baada ya kuona imetengemaa,  wawarudishe ofisi za Serikali ya Mtaa ambako wajumbe wote wana orodha ya wananchi wao. Hali hiyo ilitengamaa kwenye mitaa hiyo na amani imerejea mara baada ya juhudi za Mheshimiwa Paul Makonda.
Kufuatia hotuba ya Meya huyo, Maskanibongotz ilishuhudia akina mama wengi wakiangua vilio huku kila mmoja akizungumza lake na wengine wakisema kwa upeo wao wanaona Meya huyo amepokea vibaya taarifa toka kwa watu wake wa chini hasa viongozi wa Chadema ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa wakimnung'unikia Peter Bilebela wa CCM.
Hata hivyo, wananchi hao wamesema wamemlilia Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Paul Makonda ambaye kiukweli alikuwa upande wao kiasi cha kuwafanya warudishe imani na serikali yao waliyokuwa wanaichukia kwa kushindwa kuwatetea wanyonge. Aidha, wamemuomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi kuunda kamati toka Wizarani kwake ili washughulikie suala hilo kwa umakini na kufuata haki.
Wanasema, hiyo inatokana na kuhisi kama mgogoro huo wa ardhi kwa sasa umeingizwa mambo ya siasa ilhali tayari watu wanaojiita wenye mashamba walishaua, walishaharibu mali kwa kuwabomolea watu nyumba zao bila kibali halali cha mahakama, hivyo wanaamini maamuzi pekee yatakayotolewa na Serikali kuu yatakuwa sahihi na wataishi kwa amani kama wenzao wa Chasimba.
Source: Pazia Jeusi
Visit Youtube or Facebook for more info.
SOMA ZAIDI ...

Tuesday, June 14, 2016

HII HATARI. TIZAMA PICHA 15 ZA MASHOGA WALIONUSURIKA KIFO KWENYE CLUB YA USIKU, MASHOGA WALIOPOTEZA WAPENZI WAO WASUSA KULA NA KUNYWA SIKU YA TATU LEO, MASHOGA WA TANZANIA WAOMBOLEZA KIMYA KIMYA KUOGOPA KUJURIKANA, MASKANIBONGOTZA IMEKUWEKE PICHA ZA TUKIO ZIMA HIZO...!

0 comments
 Mmoja wa mshoga mashoha hao aliyepoteza mpenzi wake akizungumza kwa masikitiko makubwa, huku akisema amesusa kula kwa siku ya tatu hadi.
 Huyu pia akilia kwa uchungu baada ya kumpoteza mchumbaake ambae ni shoga mwenzake, kwa mujibu wa mtandao mmoja nchini Marekani unasema kijana huyu anasema tayari alishavishwa pete ilibaki kuoana tu.
Hawa ni wapenzi ambao siku ya tukio wao hawakwenda night club
 Hawa ni kati ya wale mateka waliokuwa wametekwa na muuaji Omar Mateen ambae baadae waliokolewa na polisi kisha kijana huyo kuuawa.
Miili ya mashoga hiyo ikiwekwa sawa kuingizwa kwenye majokofu.
 Hwa ni wale wanawake wasagaji ambao walinusa kifo.
Afisa Usalama toka FBI kiangalia njia alizopitia muuaji na kuingia ndani na machine gun
Mateka wakilia kwa uchungu baada ya kupoteza wenza wao ambao ni mashoga wenzao.
 Polisi wakiokota miili ya mashoga hao.
 Shoga huyu ambae nae amesusa kula wala kunywa kwa kumpoteza kipenzi chake.


Mkuu wa kitengo cha FBI kwenye jimbo la Orlando akiwasili eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi.
Hawa wakiomboleza vifo vya mashoha hao kwa staili hii.
 Omar Mateen muuaji kama anavyoonekana enzi za uhai wake. ambapo habari zaidi zilisema kuwa muuaji huyo siku moja akiwa na umri wa miaka kumi na tano akiwa na baba'ake mzazi aliwahi kushuhudia wanaume kwa wanaume wakibusiana achukuia sana kile kitu, akamwambia Baba yake kuwa iko siku atakuja kufanya kitu kibaya dhidi ya mashoga hadi ulimwengu utakuja kushangaa..!
Hapa mashoga wakiwasha mishumaa kama ishara ya kuwakumbuka wenzao.


Hata hivyo inaelezwa kuwa mashoga wa Tanzania nao wapo kwenye majonzi mazito sana ila wanashindwa kujitokeza kulaani kitendo hichi.
Source: Maskanibongotz kwa msaada wa mtandao
SOMA ZAIDI ...

Monday, June 13, 2016

VIDEO: KAMA ULIPITWA KUONA MAZISHI YA BONDIA MUHAMED AL, NIMEKUWEKEA HAPA FULL SHUGHURI NZIMA...!

0 comments
Mastaa mbalimbali wakiwa wakisukama jeneza lililobeba mwili wa Bondia Mohamed Al aliyezikwa mwishoni mwa wiki nchini Marekani..!
SOMA ZAIDI ...

VIDEO: HII NDIYO TOP 1O YA MAGOLI BORA MUDA WOTE COPA AMERIKA...!T

0 comments


Michuano maalum ya Copa America 2016 bado inaendelea, najua unajua kuwa mashindano hayo mwaka huu yanafanyika kwa lengo la kusherehekea miaka 10 ya michuano hiyo, tayari tumeshuhudia timu kama Brazil ikiaga mashindano hayo, lakini wakati tukiendelea kuburudika na michuano hiyo jikumbushe magoli 10 bora ya Copa America.
SOMA ZAIDI ...

SHUHUDIA PICHA ZA TUKIO LA MWIGULI NCHEMBA ALIVYOWASILI KUMRIDHI KITWANGWA ALIYEPIGWA CHINI NYADHIFA HIYO KISA IKIWA NI ULEVI...!

0 comments


June 13 2016 aliyekuwa waziri wa Kilimo na mifugo Mwigulu Lameck Nchemba aliapishwa rasmi Ikulu Dar es Salaam kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu ameapishwa kurithi nafasi iliyokuwa imeachwa wazi na Charles Kitwanga ambaye Rais Magufuli alifuta uteuzi wake May 2016 kwa kosa la kuingia na kujibu maswali ya wizara hiyo ikiaminika kuwa kalewa.
IMG-20160613-WA0019
Baada ya kuapishwa kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba akiwasili ofisini kwake
IMG-20160613-WA0020
SOMA ZAIDI ...

Wednesday, June 8, 2016

RC PAUL MAKONDA KIBOKO, APEWA SHAVU JINGINE LA MAANA, WAZEE NA VIONGOZI WA DINI MKOA WA DAR WATOA KAURI NZITO.

0 comments
 RC MAKONDA
  RC MAKONDA KIPINDI AKIWA MKUU WA WILAYA KINONDONI AKIWA AMEZUNGUKWA NA MABANGO YENYE JUMBE MBALIMBALI ZIKIWEMO ZA KUONDOA UFISADI WA ARDHI KWENYE KITENGO CHA MIPANGO MIJI KINONDONI AMBAO WALISHRIKIANA NA MAFISADI KUFANYA UHARIBIFU MKUBWA WA MALI BIKA KIBALI CHA MAHAKAMA HUKU WATU ZAIDI YA SABA WAKIPONEZA MAISHA.
 JOYCE ASENGA MWANAHARAKATI ASIYEKUWA NA CHAMA AMEMPONGEZA RC MAKONDA KWA UTENDAJI WAKE KAZI HASA KWENYE UTETEZI WA WATU WANYONGE AMBAO WALIKUWA WAMEKOSA MATUMAINI NA SERIKALI YAO.

Na Livingstone Mkoi
 Nyota ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda imeendelea kung'ara baada ya wakazi wa kata ya Wazo mtaa wa Nyakasangwe na Nyakalekwa kuiomba Manispaa ya Kinondoni kuruhusu mitaa hiyo kuitwa jina la Makonda kutokana na kazi kubwa aliyoifanya wakati akiwa mkuu wa Wilaya hiyo.

 Wakiongea na Maskanibongotz/ Sadicktv wakazi wa maeneo hayo kwa nyakati tofauti walisema ‘Mheshimiwa Makonda amefanya jambo kubwa sana  kurejesha amani  iliyokuwa imepotea hadi kusababisha maafa kwenye mgogoro wa ardhi katika eneo letu’ , eneo hilo awali lilikuwa na vita ya wakazi na watu wanaojiita wenye mashamba ilikuwa vita ya kutumia siraha za jadi kama mishale, mapanga na visu baina ya watu wanaosadikika kumiliki maeneo makubwa na wakazi ambao wamekuwa wakiishi hapo kwa muda mrefu,kitu ambacho kilipelekea hata jeshi la Polisi kushindwa kuthibiti kwa wakati.

Baada  ya kuteuliwa Ukuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda  ziara yake ya kwanza ilikuwa eneo hilo ambapo siku ya kwanza alifika katika eneo hilo na gari zisizopungua saba za Polisi na kufanya mkutano  katika viwanja vya Shule ya msingi ya Wachina ambapo aliwaaahidi wakazi hao kuwa atapigana kufa na kupona kuhakikisha wakazi hao wanapata haki yao ya kupata ardhi lakini na kurejesha amani iliyokuwa imepotea.

 Makonda alianza kuunda kamati iliyoshirikisha sehemu tatu, moja ilikuwa ni ya watu wanaojifanya wenye mashamba, mbili ya wakazi wa eneo hilo na tatu iliyokuwa chini yake na baadaye alikaa chini kukubariana wafanye uhakiki kwanza wa maeneo hayo ili kubaini ni kweli watu hao wenye mashamba wanachokisema kuhusu ukubwa wa maeneo yao ni sahihi.

Zoezi la kuhakiki lilianza mwaka jana lakini ikabainika madudu makubwa kwani watu wanaosema hayo ni mashamba yao walionekana kufanya udanganyifu wa hali ya juu kwa kile kilichoonekana kwamba wamejiongezea maeneo kinyemela tofauti na vile ambavyo inaonyesha katika michoro, hivyo kupelekea kazi sasa kuwa rahisi kugawa haki kwa wakazi wa eneo hilo.

 Hata hivyo  zoezi hilo kwa sasa limesimama tangu Makonda apande cheo huku wananchi wote wa eneo hilo masikio yao, macho yao na akili  zao zipo kwa Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ndiye wanayemtegemea kutatua tatizo hilo, huku wakiamini ya kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watu hao wenye mashamba kwa mambo matatu, la kwanza walisababisha mauji ya watu saba wakati wa mapambano kipindi walichokuja kuvunja eneo hilo, na suala jingine ni nani aliyewapa mamlaka ya kuwavunjia watu nyumba zao pamoja na kuharibu mali zao zenye thamani ya mabilioni ya pesa na la mwisho uongo wa kumdanganya Makonda na vyombo vya sheria.
Kwa sasa hali ni shwali katika eneo hilo, kinachosubiriwa ni hatua zichukuliwe dhidi ya waharibifu, lakini amani ambayo wanaipata Wananchi wa eneo imewafanya watoe ya moyoni kwamba pasipo Paul Makonda hawajui mpaka leo wangekuwa katika hali gani ‘Tulijiona si Watanzania tena, Makonda ametufanya tufurahie amani ya nchi yetu, kwa sasa tunaishi kwa amani sana, tunaomba Serikali itusikie, hatuna cha kumpa Makonda, lakini ni heshima kwetu kuona eneo hili linapewa jina lake, hii itatosha kuwaambia watu wote na vizazi vijavyo kazi nzuri aliyotufanyia Kijana huyu’, walisema Wazee wa eneo hilo.

Katika hatua nyingine Viongozi wa Dini wa eneo hilo, wamesema ya kwamba kuna wakati Mungu anawatumia watu wake kuokoa, kwa nyakati tofauti Viongozi hao wamesema unaposoma maisha waliyoishi mitume na manabii, utapata kuona jinsi ambavyo walitumwa na kupambana pale inapotokea kwamba eneo fulani linakosa amani, eneo hili awali Mkuu wa Mkoa aliyepita Mecky Sadick alikuja lakini hakuweza kumaliza tatizo, tumeona alichofanya Paul Makonda, tunasema huyu alitumwa kuhakikisha anarejesha amani ya Nyakasangwe na Nyakalekwa, tunamuombea kwa Mungu na hakika anastahili heshima hii ambayo wakazi wa eneo hili wameamua kumpa, alisema Mchungaji Mzola wa Kanisa la Mlima Sayuni Nyakasangwe.
Source Maskanibongotz
SOMA ZAIDI ...

Saturday, June 4, 2016

RC MAKONDA AWASHANGAZA WATU KWA MAMBO YAKE ANAYOYAFANYA, WAMSHAURI KITU RAIS JOHN POMBE MAGUFULI KUTOKANA NA TABIA HIYO YA MKUU WA MKOA..!

0 comments
 Mkuu wa Mkoa wa Dsm Mheshimiwa Paul Makonda
Umati wa mashabiki ukimsikiliza Mheshimiwa Paul Makonda ambaye hayupo pichani.
Na Livingstone Mkoi
 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dr Pombe John Magufuli hakufanya kosa kumchagua Paul Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutokana na utaofauti wake na wakuu wa mikoa mingine.
Hilo limedhihilika jana kwenye viwanja vya Posta Kijitonyama katika hali isiyotarajiwa Mheshimiwa Paul Makonda alijichanganya na vijana wa bodaboda na bajaji pamoja na mashabiki wa muziki wa Singeri waliokuwa wamefurika viwanjani hapo hadi kukosekana nafasi ya kupita.
Makonda ambae ana histori ya kutokupenda mbwembwe kwenye misafara yake tofauti na wakuu wengine wa Mikoa ambao hupenda kuandamana na misafara ya polisi kwa mbwembwe aliingia kwenye viwanja hivyo jioni majira ya saa kumi na nusu huku akiwa na mlinzi wake tu.
Kitendo hicho cha mkuu huyo wa mkoa kujichanganya kwenye show za hali ya chini kimewashangaza watu na kusema Makonda anatakiwa kuwa mfano kwa wakuu wote wa Mikoa kuiga tabia kama yake ya kuwajar watu wote bila kujari wa hali ya juu ama ya chini.
Kutokana na mambo hayo ya Makonda kuwa mfano mzuri kwenye jamii, watu mbalimbali waliofika uwanjani hapo kwenye onesho la Komaa Concert lililohudhuliwa na watu wasiopungua elfu 45 walimshauri Mheshimiwa Rais kwenye uteuzi wake wa wakuu wa Mikoa ateue watu wenye sifa kama Makonda asiyekuwa na makuu.
Ujio wa Makonda uwanjani hapo uliwashuta hata maafisa wa Polisi toka kituo cha Polisi Oysterbay ambao hawakutegemea kama Mheshimiwa Makonda angeweza kuja uwanjani hapo kujichanganya na vijana wa hali ya chini, ghafra walimuona tu akitunda dunda viwanjani hapo akiwa na mkuregenzi wa kituo cha E-fm Radio Bwa Francis Siza "Majey"  
SOMA ZAIDI ...

MCHUGAJI WA AJABU ANAEPONYA WAGONJWA WA UKIMWI, KISUKARI, VICHAA AZIDI KUWASHTUA MADAKTARI BINGWA, JIJI LA DAR LAHAMIA WAZO KANISANI KWAKE KUPATA UPONYAJI WA PAPO KWA PAPO...!

0 comments

Mmoja wa wagonjwa ambae ameacha kitanda na kwenda kwa Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Lililopo Nyakasangwa kata ya Wazo kwa ajiri ya kupata huduma ya uponyaji wa kweli.

 Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Msigani maarufu kwa jina la  NGOMA YA YESU MSIGANI lililopo Wazo Jijini Dar


Na Mwandishi Wetu
Hakika Mungu hutumia watumishi wake kufanya maajabu, hivi ndivyo tunavyoweza kusema. Mchungaji wa Kanisa la Hosana Msigani, Mzola ameendelea kuushanga ulimwengu kutokana na nguvu ya ajabu aliyokuwa nayo ya kuponya watu wenye magonjwa sugu yakiwemo Ukimwi, Kansa nk.
Mchungaji huyo mwenye kanisa dogo tu lililopo Waza mtaa wa Nyakasangwe Msigani lakini amekuwa akifanya mambo ya kushangaza watu kutokana na nguvu ya upako aliyokuwa nayo.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wagonjwa wengi kwa sasa toka Hospitali mbalimbali za Jijini Dar na nje ya Dar wenye magonjwa yaliyoshindikana  wameamua kuacha vitanda na kukimbilia kwa amchungaji huyo tena wakiwa kwenye pikipiki kwa msaada lakini wakanyagapo kwenye ardhi ya kanisa hilo tu, basi hupata uponyaji wa papo kwa hapo.

Hata hivyo mchungaji huyo amewaomba watanzania popote walipo Duniani wasisubiri kifo kiwakute kwa matatizo yanayowasumbua na hata kwa magonjwa sugu kama Ukimwi, Kansa, kichaa, Ugumba, kutokupata mafanikio kwenye biashara  nk wawabebe watu wao na kumlekea ili awape dozi ya Yesu Kristo kwani lisilowezekana kwa binadamu linawezekana kwa Mungu.
Mchugaji aliongeza kusema" Wabebeni wagonjwa wenu na kuwaleta hapa kwenye dozi isiyokuwa na gharama Mungu hashindwi jambo" Alisema na kutoa namba yake ya simu 0713-161785 kwa watu wasioweza kufika kanisani kwake atawapatoa dozi hiyo kwa njia ya simu na watapokea uponyaji huko huko walipo bila gharama yoyote.
SOMA ZAIDI ...

Sunday, May 29, 2016

MSANII AFANDE MACHEMBA AWACHANGANYA MASTAA WA KIKE BONGO MIVE, YUPO CHUCHU HANSI. RAY MMH...!

0 comments
AFANDE MACHEMBA AKIWA MZIGONI NA CHUCHU HANS, AMBAPO MSANII HUYU WA KIUME AMEONEKANA KUWA NA NYOTA YA AJABU KWENYE TASNIA YA BONGO MOVIE KUTOKANA NA KIPAJI CHA HALI YA JUU ALICHOKUWA NACHO.

AFANDE MACHEMBA.
Na Mwandishi Wetu
Kitendo cha mastaa mbalimbali wa filamu Tanzania kutaka kufanya kazi pa1 na msanii chipikizi anaekuja kwa kasi ya kimbunga kwenye tasnia hiyo Joseph Machemba " Afande Machemba" kimeendelea kumuweka kwenye wakati mgumu msanii huyo.
Akiongea na maskanibongotz Machemba alisema " Kaka hakika Mungu ni mwema na sijui nimpe nini huyu Mungu wangu kwa matendo yake makuu hadi nashangaa kwa baraka zake ambapo licha ya uchanga wangu kwenye tasnia hiyo lakini napata kazi kubwa ambazo zote naigiza na mastaa ambao kiukweli hakuna asiyekubari kazi yangu" Alisema Machemba
Msanii huyo ambae ni msukuma wa Shiyanga aliongeza kusema hali hiyo ya kupata kazi kila siku imemfanya kuwa busy na uigizaji kiasi cha kukataa kazi za watu wengine kutokana na ratiba inavyombana.
Afande Machemba aliendelea kueleza kuwa hadi sasa ameshacheza filamu nyingi na tayari mlango wa mafanikio ameanza kuuona " Kaka msema kweli mpenzi wa Mungu tayari nimeanza kuonja mafanikio ya sanaa nilianza kucheza filamu bure lakini kwa sasa nalipwa tena naweza kusema hela ndefu, nina washukuru wasanii wenzangu hasa mastaa wote hakuna ambae hanikubari kila filamu natakiwa nishiriki" Alisema msanii Machemba hadi sasa ameshacheza filamu nyingi sana ikiwemo Chobo Dundo, Smart Phone, Handsome Fake, na nyingine ambazo zote zipo madukani na yeye akiwa ametumia jina la Afande Machemba.
CHUCHU NA RAY
SOMA ZAIDI ...

Monday, May 2, 2016

RC MAKONDA KIBOKO, MAFISADI WA ARDHI KATA YA WAZO WAINGIWA HOFU YA KUKAMATWA, NI WALE WANAOKABIRIWA NA KESI YA KUUA WATU, KUHARIBU MALI ZA WANANCHI WANYONGE, KUIDANGANYA MAHAKAMA...!

0 comments
 DC Makonda akipokewa na mabango ya kuwakataa maafisa Ardhi Manspaa ya Kinondoni wanaidaiwa kuwa karibu na mafisadi hao
 Hapa picha hii Makondo akiwa amekaa chini siku ya kwanza alipotembelea Nyakasngwe akiwa DC

Na Mwandishi wa Maskanibongo- Wazo
Hakika serikali ya awamu ya tano imerejesha matumaini mengi ya watanzania hasa wanyonge waliokuwa wanaonewa na watu wenye fedha zao makusudi huku wakikosa mahara pa kukimbilia, huku wananchi wengine  kupoteza maisha kwenye harakati za kutetea haki zao, moja ya eneo ambalo lilikuwa na vita kubwa ni Nyakasangwe kata ya Wazo ambalo mafisadi walilitumia kuwafanyia watu umafia wa kutisha.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda wakati akiwa bado mkuu wa Wilaya ya Kinondoni aliingilia kati sakata la mgogoro huo wa ardhi kati ya watu wanaojiita wenye mashamba na wananchi wakati wa eneo hilo kupitia maamuzi yake alifanikiwa kurudisha amani iliyokuwa imepotea muda mrefu kwenye eneo hilo.
Makonda atakumbukwa na wananchi wanyonge wa eneo hilo kwa kuwatetea na kuwatia moyo wakati akiwa mkuu wa Wilaya hali hiyo iliwafanya watu wanaodai ni wamiliki wa mashamba hayo kumuangalia kwa jicho mbaya Makonda kwani awali mafisadi hao walizoea kuwatumia viongozi wa Serikali hasa wa awamu iliyopita kwa kutoa rushwa ili wawakatandamize wananchi.
Makonda katika sakata hilo alionesha msimamo wake hali iliyopelekea mafisadi hao kumuogopa sana huku wengi wao walianza kuyaacha wazi maeneo hayo ili wananchi hao waendelee kuishi kwa amani na utulivu.
Hata hivyo kwa sasa hali imekuwa mbaya licha ya kwamba kesi ya mgogoro huo wa ardhi ipo mahakamani, upande wa pili mafisadi hao wameingiwa na hofu ya kukamatwa kwa mambo matatu, Jambo la kwanza wana kesi ya kuidanganya mahakama kwa kusema wanamiliki maeneo yenye ukubwa flani lakini kumbe ni uongo. jambo la pili katika mgogoro huo kuna wananchi wanyonge walipoteza maisha na jambo la tatu mali zao ziliharibiwa na polisi huku kazi hiyo ikifanywa na mafisadi hao.
Hivyo kutokana na hali hiyo imelezwa kuwa mafidi hao kwa sasa wanaomba kuyamaliza nje ya mahakama ili kukwepa kitanzi hicho, ambapo imelezwa tayari Makonda ana ripoti yote kwa sasa mezani na amebakisha kufanya maamuzi magumu juu ya mafisadi hao kwani hawakuwa na kibali toka mahakamani kuwabomolewa wananachi hao na kuharibu mali lakini na kusababisha maafa kwa wananchi.
Makonda ambae kwenye mgogoro huo wakati akiwa mkuu wa wilaya alishindwa kufanya maamuzi kutokana na vikwazo flani vilivyokuwepo toka kwenye ofisi ya mkuu wa Mkoa aliyepita ambapo ilidaiwa kuwa ilikuwa anahusika na mgogoro huo hivyo hali ilimfanya Makonda kushindwa kufanya maamuzi ya mwisho lakini kwa sasa kapewa rungu na mheshimiwa Rais  la kufanya maamuzi watanzania wengi wanatarajia kuona mafisadi hao wakichukuliwa hatua kali.
Source: maskanibongotz

SOMA ZAIDI ...

Thursday, April 7, 2016

MUNGU MKUBWA: SHOGA ALIYEOKOKA NA KUMPOKEA MUNGU AELEZA JINSI ALIVYOACHANISHA NDOA YA MTU KISHA KUOLEWA NA MUME HUYO, MASKANIBONGOTZ

0 comments
 ANT ASU ENZI HIZO WAKATI BADO AKIJISHUGHURISHA NA USHOGA AKIWA KATIKA POZI  SIKU YA SENDO OFF YAKE ILIYOFANYIKA NYUMBANI KWAKE KWENYE KOTA ZA MAGOMENI KABLA HAJIZAVUNJWA.
 ANT ASU AKIWA KWENYE POZI
KIJANA AMBAE NI BAUNSA MAARUFU JIJINI DAR AMBAE ALIAMUA KUMUACHA MKEWE NA KUMUOA SHOGA HUYO PICHANI JUU.
Na Mwandishi wa Maskanibongotz
Hakika Mungu ni mkubwa hivi ndivyo tunavyoweza kusema kwani  hizi taarifa ni vyema kuzisikia kwa mtu mwingine na si kwa mtoto wako.
Naamini familia ya kijana huyu ambae amekuwa akijishughurisha na ushoga kwa miaka mingi hadi kuolewa na kuishi na mwanaume kwa miaka 6 ndani.
Huyu ni kijana ni maarufu sana hapa mjini anaitwa Ant Asu ambae kwa sasa huenda akawa ameipa ahueni familia yake na watu wa karibu kufuatia kuokoka na kuachana na mambo ya kishoga.
Akiongea na maskanibongotz kijana huyo alisema" Namshukuru Mungu kwa kweli kwa sasa naendelea vizuri nimeachana na hiyo tabia kwa sasa sitamani na nina umia sana nikikumbuka nilivyoiba wanaume za watu na kuwapagawisha kwa kuwapatia mapenzi motomoto" Alisema
Kijana huyo anaendelea kuieleza maskanibongotz alisema" Niwaombe radhi wanawake za watu kwa kweli hasa wanaoishi magomeni kwani walikuwa hawapumui wakiniona, lakini kwa sasa nimeokoka na nimekuwa mtu mwema na nahitaji maombi zaidi ili niendelee kuwa na hofu ya mungu na pia naimba radhi familia yangu najua imeumia kwa muda mrefu ila nimeamia kwa Mungu hakuna lisilojulikana' Alisema
Credit; Maskanibongotz
SOMA ZAIDI ...

RAIS MAGUFULI KIBOKO, ASAFIRI HADI RWANDA KWA GARI, AZIDI KUSHIKA UMAARUFU KWA KUSIMAMIA KAURI ZAKE ZA KU MINIMIZE BAJETI, ANGALIA PICHA HIZI HAPA..!

0 comments
.
.
Ni safari ya kwanza ya nje ya nchi kwa Rais Magufuli toka alipoteuliwa kuwa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania October 2015, kasafiri kwa gari kwenda Rwanda ambapo kwenye siku yake ya kwanza yeye pamoja na Rais Kagame wamezindua daraja la Rusumo kwenye mpaka wa Tanzania na Rwanda. 
.
.
.
.
.
.
.
.
.
ULIIKOSA YA RAIS MAGUFULI KUNUNULIA WATU SODA MWANZA NA YEYE KUKAA KULA KWENYE MGAHAWA? TAZAMA HII VIDEO HAPA CHINI

SOMA ZAIDI ...

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king