Thursday, March 9, 2017

HALI YA HATARI; RAIS MAGUFUL NA WAZIRI LUKUVI WANTED, JESHI LA POLISI LATAHADHARISHWA, WABAYA WATAKA KUTUMIA SAKATA LA MAKONDA KUFANYA UMAFIA…!




Na Livingstone Mkoi- Maskanibongotz
 
Wananchi wa mtaa wa Nyakasangwe na Nyakalekwa wanaoishi kwenye mgogoro wa ardhi kwa zaidi ya miaka kumi na tano sasa wameingia hofu kuhusu hatma ya makazi yao dhidi ya mafisadi wa ardhi ambao tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda aingie kwenye sekeseke la tuhuma za vyeti batili.

Wakiongea na waandishi wetu wa mtandao wa Maskanibongotz wakazi hao wapatao elfu nne walisema  tangu ishu ya Makonda ilipozuka watu hao wanaodai wenye mashamba wamekuwa wakionekana karibu kila siku wakiwa na magari ya kifahari katika makazi yao jambo linalowapa hofu kubwa.

Hofu waliyonayo wakazi hao ambao hadi sasa wameshahakikiwa katika eneo hilo na kubakisha kupewa hati za Serikali tu ili wayamiliki kihalali makazi yao, wamesema wasi wasi huenda watu hao wenye mashamba ambao “ Mafisadi Ardhi” Wakatumia udhaifu wa matatizo ya Makonda kuwaonea mwanzo jinsi walivyobomolewa makazi yao bila kibali cha mahakama huku watu kumi na tatuu wakipoteza maisha.

RC Makonda ndiye aliyekuja kusambaratisha mtandao huo wa ufisaidi na kufanikiwa kuwaweka huru wakazi hao ambapo awari watu waliokuwa wameyaterekeza mashamba hayo zaidi ya miaka ishirini na kuacha msitu huku majambazi wakitumia maficho ya uharifu hadi Mkuu wa Mkoa miaka hiyo Yusuph Makamba alipoamuru Serikali ya mtaa kugawa eneo hilo.

Watu hao wenye mashamba walijaribu kutumia nguvu kubwa ya kifedha kuwaondoa  wananchi kwa kutumia Polisi, wenye sialaha, na mabomu, na mabaunsa kwa kuwabomolea hadi kupelekea wakina mama kujifungua kabla ya muda, huku wengine wakipoteza maisha, walifanyiwa ukatili huo bila msaada wowote katika utawala uliopita hadi alipokuja Makonda kurudisha amani.

Makonda alionekana adui mkubwa dhidi ya mafisadi hao kiasi cha kumchukia kwa kuwatetea wananchi hao wanyonge, katika neo hilo palikuwa hapaingiriki zaidi ya kuwindana na mishare ya sumu kwa wananchi na bunduki kwa Polisi, ilifika mahara wakazi hao walipewa kesi  kuwa wao sio raia wa Tanzania kwa lengo la kuwaondoka tu, lakini kipindi cha kupiga kura wananchi hao waliachwa kwa muda ili wapige kura baada ya kumalizika  kupiga kura waliisoma namba.

Baada ya maongezi na wananchi hao waandishi wetu walifika ofisi za Serikali ya mtaa wa Nyakasangwe zinazoongozwa na Mtumishi wa Mungu Peter Bilebela kwa ajiri ya kupata ukweli wa jambo hilo.

Mwenyekiti huyo alianza kuzungumzia jambo hilo “ Kwanza kabisa niwashukuru ndugu waandishi kwa kufika huku kwetu kujionea hali halisi, kuhusu hizi taarifa za kuonekana kwa watu hao ndani ya magar ya kifahari ninazo licha ya kwamba mimi sijafanikiwa kuwaona kwa macho yangu” Alisema

Kiongozi huyo aliongeza kusema” Kwa vile wananchi wangu ndiyo wapo huko mtaani naamini kabisa taarifa hizo ni za kweli kwani katika mitaa yetu tunaishi kwa ushirikiano mkubwa hivyo wanapoona kitu tofauti lazima watanifikishia taarifa hizo” Alisema
Hata hivyo mwenyekiti huyo aliongeza kusema kuwa wananchi wake kweli wapo kwenye hofu kubwa juu ya hatma ya Makonda ambaye kwao wanamchukulia kama shujaa kutokana na alichokifanya katika mitaa hiyo kwa kurudisha amani iliyokuwa imetoweka miaka mingi iliyopita.

Mwisho, Mwenyekiti huyo kwa niaba ya wananchi wake ambao wamekuwa wakimsumbua kila siku wakiwataka  viongozi wakuu wa nchi  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi nchini, Mhe. William Lukuvi  siku moja wafike katika mtaa wao huo wa Nyakasangwe kata ya Wazo.  Kumaliza mgogoro huo ili wananchi waanze kulipa kodi za viwanja  na majengo kwani Serikali inapoteza mamilioni ya shilingi kwa kukosa kukusanya kadi kutokana na uchelewaji wa kuwapimia wananchi viwanja na kupewa hatimiliki.

Lakini pamoja na hayo wakazi hao wameomba  Jeshi la Polisi kuweka tahadhari juu ya  watu hao wenye mashamba kwani wakijaribu kufanya jambo kuleta uvunjifu wa amani hali inaweza kuwa mbaya kwani safari hii hawatokubari kuonewa kama walivyofanya kwa utawala wa Rais Kikwete na kusisitiza huu ni utawala wa Magufuli ambao hautaki uonevu na upo kwa ajiri ya wanyonge.
Source: Maskanibongotz
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi nchini, Mhe. William Lukuvi

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king