Sunday, October 19, 2014

SINA MPANGO WA KUOLEWA TENA. DIDA ASEMA WANAUME WANAZINGUA SANA...!


NDOA basi! Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amezima ndoto za kuishi maisha ya mke na mume kwa kudai kuwa, amebaini kujiingiza kwenye ulimwengu huo ni kujipa ‘stress’ za kujitakia.
Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda juzi, Dida alisema baada ya kuachana na aliyekuwa mume wake, Edzen Jumanne, amebaini wanaume wote lao ni moja hivyo kama atakubali kuingia kwenye ndoa na mwanaume mwingine, itakuwa ni yaleyale.
“Yani sasa hivi hata aje mwanaume na gia gani siwezi kukubali kuolewa tena, kwa kifupi sina ndoto za kuitwa mke wa mtu tena, bora nibaki peke yangu nifanye mambo yangu,” alisema Dida.

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king