Tuesday, October 13, 2015

HII KUFURU YA PESA: TIZAMA PICHA ZA BONDIA FLOYD MAYWEATHER AKILA BATA NA RAFIKI ZAKE WATUMIA ZAIDI YA DOLA ELF 50 USIKU MMOJA..!


Bondia mwenye rekodi ya kutopigwa Floyd Mayweather bado anaendelea kufanya matanuzi ya mkwanja wake aliyovuna katika mchezo wa ngumi. Floyd Mayweather ambaye mwezi September alimpiga kwa point bondia Andre Berto pambano lililofanyika katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena Las Vegas Marekani.
2D51CE0600000578-0-image-a-6_1444638786158
Mayweather Jr alipigwa picha akiwa katika bwawa la kuogelea Miami sambamba na uwepo wa rafiki zake, huku akionekana kujiachia zaidi dalili ambazo zinaashiria kuwa hana pambano hivi karibuni kwani muda mwingi ameonekana akiwa anaenjoy na rafiki zake.
2D51CE1500000578-0-image-a-1_1444638654935
Bingwa huyo wa uzito wa kati hadi sasa ana rekodi ya kupigana mapambano 49 na kutopoteza pambano hata moja kati ya hayo. Hata hivyo kuna stori zinazozungumzwa kuhusu promota maarufu wa mchezo wa ngumi Bob Arum kutaka kuandaa pambano la marudiano kati ya Mayweather Jr dhidi ya mpinzani wake Manny Pacquiao.
2D51CE0E00000578-0-image-a-5_1444638778961

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king