Monday, October 27, 2014

UKAWA WAWASIHI VIJANA KUJITOKEZA KWA WINGI ILI WAJIANDIKISHE KWENYE DAFTARI LA KUPIGA KURA ILI 2015 WAING'OE CCM NA MAFISADI..!


Wabunge wa TZ, ambao baadhi yao wa upinzani wameungana, kuing'oa CCM.

Upinzani nchini Tanzania umetia saini makubaliano ya pamoja, kuking’oa madarakani Chama tawala.
Utiaji huo saini makubaliano ya kukishinda Chama cha Mapinduzi CCM, katika uchaguzi ujao, umefanywa na viongozi wa vyama vinne, huku tukio hilo likishuhudiwa na wafuasi wao.
Katibu Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Dr. Willibrod Slaa ni miongoni mwa viongozi waliotia saini makubaliano hayo na amesema vyama hivyo vitasimamisha wagombea wake kwa pamoja kwenye ngazi zote za uchaguzi kuanzia serikali za mitaa mpaka ngazi ya urais.
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim seif Sharif Hamad anasema tukio hilo la vyama kusaini makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kuing’oa CCM ni muhimu na la kihistoria.
Viongozi waliotia saini waraka huo wa makubaliano ni Freeman Mbowe Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Profesa Lipumba Mwenyekiti wa Chama cha wananchi CUF, Katibu Mkuu wa Chama hicho ambaye pia ni Makamu wa kwanza rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, James Mbatia Mwenyekiti NCCR Mageuzi, Mosena Nyambabe Katibu Mkuu NCCR Mageuzi, Dr Emmanuel Makaidi Mwenyekiti NLD na Tozzi Matwanga Katibu Mkuu wa NLD.

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king