Thursday, January 1, 2015

MOVIE YA EXPENDABLES YA KITANZANIA KUTIKISA 2015 IMEWASHIRIKISHA MASTAA ZAIDI YA 30 WA BONGO MOVIE NI YA MSANII MANAIKI SANGA ICHEKI HAP LIVE..!

 Msanii nyota Kajala Masanja akiwa na msanii wa bongo flava na filam nchini wakiigiza filamu hiyo Mkoani Arushsa hivi Karibuni.
 Staa wa filamu ya Wake Up Manaiki Sangu akiwa mbele ya mastaa mbalimbali walishiriki filamu hiyo ambayo imefananishwa na ile ya Expendables ya nje kwa kusheheni mastaa zaidi ya 30 huku wakiwa wamechuana vikali.
 Kazi kazi wasanii Hemed Suleiman na Irene Uwoya wakiwa kwenye hisia kali wakati wakiigiza filamu hiyo ya Wake Up ya msanii Manaiki Sanga " The Don"
 Mzee Majuto ambae amekuwa kivutio kikubwa ndani ya filamu hiyo ya Wake Up

Na Mwandishi Wetu
Msanii wa Bongo Movie na Bongo Flava nchini Manaiki Sanga amefanya kitu ambacho hakikuwahi kufanyika nchini toka 15 iliyopita tangu sanaa ya filamu ilipoanza baada ya kuandaa filamu iliyowakutanisha wasanii zaidi ya 30 ndani ya filamu moja.

Akiongea na gazeti hili muongzaji filamu hiyo Leah Richard Mwendamseke “Lamata” Alisema kuwa filamu hiyo ambayo maandalizi yake yamemaliza miezi sita hadi kukamilika kuigizwa kwake huku akimpa wakati mgumu sana na kuwa historia kwake tangu aanze kuongoza filamu za nchini Tanzania.
Lamata aliwataja mastaa walioshiriki filamu hiyo iliyopewa jina la “Wake Up” Irene Uwoya, Jackline Wolper, Gabo,  Othuman Amri “King Majuto” Kajala, Yusuph Mlela, Tausi, Aisha Boko, Hemed Suleiman, Quickrocker, Kupa,Duma, Mama Abdul, Flora Mvungi, kwa upande wa wanaumziki ni Country Boy, Nas B akiwemo mwenyewe Manaiki Sanga ambae ndiye staa wa filamu hiyo.
Hata hivyo kwa mujibu wa msemaji wa msanii Manaiki Sanga Bwana Livingstone Mkoi alisema kuwa filamu hiyo kwa sasa ipo kwenye hatua za mwisho “ Tuko hatua za mwisho kumalizia na tayari tumepewa ofa kibao za kuiuza filamu hiyo iliyosheheni mastaa hao na kampuni mbalimbali za usambazaji filamu zimeanza kupanda dau la kusambaza filamu hiyo ya kwanza nchini Tanzania kwa kuchezwa na mastaa wengi huku ikifananishwa na ile ya Expendables ya  nje ya nchi" Alisema Mr Mkoi

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king