Thursday, January 8, 2015

MASTAA BONGO MOVIE WAMTETEA MANAIKI SANGA KUHUSU PICHA ZA UCHI!










Wasanii mbalimbali wanaunda kundi la Bongo Movie nchini ambao wameshiriki kwenye filamu ya msanii Manaiki Sanga iitwayo Wake Up wamemtetea msanii mwenzao kuhusu kashfa ya picha za uchi alizowahi kupiga miaka ya nyuma.
Wakiongea na gazeti hili hivi karibuni wakati wakiigiza filamu hiyo iliyowashirikisha zaidi ya wasanii 36 walisema kuwa binadamu wote wanatakiwa kusahau madhambi ya mtu kwa vile yalishapita ni vyema watu wakaangalia ya sasa na yajayo.
Wasanii hao ambao ambao kila mmoja aliongea jinsi anavyoona lakini kila mmoja alionekana kumtetea Manaiki kwa tukio alilowahi kulifanya.
 Mmoja wasanii hao ambae nae ni mshiriki ni Jackline Wolper baada ya kuulizwa na mwandishi wetu anazungumzia matukio ya ukatili ya msanii huyo kwa wanawake aliyowahi kuafanya ambapo alijisema “ Kiukweli Manaiki aliwahi kuteleza kama ambavyo angeweza kuteleza binadamu mwingine au mimi na wewe hivyo ni vyema tuka sahau hayo tusiendelee kumuhukumu Manaiki kwa madhambi yaliyopita si vizuri” Alisema Wolper
Aidha nae Irene Uwoya ambae aliwahi kutuhumiwa kutembea na Manaiki yeye alisema hivi “ Ndugu yangu mimi upande wangu naweza kusema kuwa jamii inapaswa kumsamehe Manaiki sisi sote ni binadamu na tunakosea ni vyema tukasahau yaliyopita tayari picha ziko mitandaoni na kama anavyoeleza mwenyewe alipoteza  Computer yake na kulikuwa na picha zake za sili” Alisema Uwoya
Mzee Majuto ambae ni swahiba mkubwa wa Manaiki alisema “Mwanangu binadamu hatujakamilika Manaiki si kijana mbaya ndiyo maaa unaona wasanii wote hawa tunampa sapoti amekuwa na ushirikiana na wenzake sana, kuhusu hizo picha ni jambo la kusahau kwa vile lilishapita tugange yajayo watanzania subirini kuipokea filamu yake mpya inaitwayo Wake Up ambayo ni kama zawadi kwa watanzania” Alisema msanii huyo mkongwe
Kajala Masanja ambae kwa sasa wameingia mkataba na Manaiki kwa ajili ya kufanya kazi pamoja yeye upande wake alisema “ Ni kweli kati ya watu walioumia sana kuona zile picha ni mimi Manaiki ni kama mdogo wangu ndiyo maana nimeamua kumchukua na kuwa nae pamoja na kumuweka sawa kisaikolojia kwa vile tayari zile picha zilikuwa zimemuathiri “ Alisema Kajala
Wasanii karibia wote walioshiriki filamu hiyo yaExpendables ya Tanzania iitwayo Wake Up iliwashirikisha wasanii zaidi ya thelathini na sita huku iliongozwa na Lamata na kushutiwa na kampuni ya Manaiki Production iliyopo Itumbi Hotel.
Wasanii walioshiriki filamu hiyo  ya Wake Up ni Irene Uwoya, Jackline Wolper, Gabo, Othuman Amri “King Majuto” Kajala, Yusuph Mlela, Tausi, Aisha Boko, Hemed Suleiman, Quickrocker, Kupa,Duma, Mama Abdul, Flora Mvungi, Tracy Moshi,  Hemed Kavu “HK”  kwa upande wa wanaumziki ni Country Boy, Nas B, Kiss, Juta B,   akiwemo mwenyewe Manaiki Sanga ambae ndiye staa wa filamu hiyo na wengine wengi.  

0 comments:

Post a Comment

.

 

Copyright © MASKANI BONGO Design by Livingstone Mkoi | Blogger Theme by BTDesigner | Powered by seleman king